Tulitoka mwanza siku ya jumatano ya tar, 23/3/2011 asubuhi ya saa nne tulipita njia ya NDABAKA Tukaanza kukata pori la Serengeti,tulipita kwenye mto wa viboko unaoitwa HIPPO POOL. TWENDE SASA!!!!
Hao ni viboko wametulia ndani ya maji tope.
TWENDE SASA!!

Soma mwenyewe!! hicho kibao kipo hapo jirani ya mto

Shost barabara mvua ikinyesha ni balaa tupu.tulikuta majuzi yake magari yalicheza rumba ya kutosha hapa TWENDE SASA!!

Kipenzi changu Conso yulikuwa pamoja baridi ilitutandika kisawasawa

Hatimae tulifika Wasso Loliondo. Nilivyoona hiki kibao kimeandikwa
LOLIONDO NILIPATA MATUMAINI KUWA TUMEFIKA,SHOST SIKUJUA KAMA NDIO KWAAAANZA SAFARI IMEANZA

Tulisogea kama kilomita 65 hivi tukakutana na foleni ya kanda ya ziwa,Shost hapa bado hatujazikuta gari za Arusha, Hapa tulilala mpaka morning bila kusogea.TWENDE SASA!

Asubuhi tulisogea kiduuuuuchu!! tukawa makutano ya arusha na kanda ya ziwa,Hapa sasa ndio usiseme mbuzi anauzwa laki 250,000 na akichinjwa kabla hajachunwa ngozi ameisha,wa mguu,kichwa,mbavu,utumbo shost hadi miguu inagombaniwa,

Njiani tulikutana na gari kibaaao zimeharibika na wenye nazo wamezitelekeza kwa uchovu.

Kule hakuna cha mdosi wala mdhungu,gabacholi, machinga kama mimi,maskini yani shost wooote ni foleni.

Shost tulisogea tena baada ya siku mbili tukawa kwenye kijisenta kipo kati hapo, TUKO PAMOJA???????

Hapo tulidodaje!! mtandao ulikuwa tabu wee acha kabisa,hapo machinga nimependa juu ya mti nipate kujua umachinga huko nyuma vipi.

Shost tairi zilikuwa zikijazwa upep0 na ile ya kujazia pikipiki,Upooo?

Hooooooooi! matumaini yanapotea kila dakika shost.

Eee bwana ee! sisi tulienda kisisita duu tukabeba maji na tubiskuti kumbe wenzetu walibeba majiko, ndizi,dagaa,unga,na vikorokoro vyooote kama unavyoona mwenzetu hapo anaandaa lanchi,

SHOST HAPA SASA!!UNAJUA KWA BABU HUTAKIWI KWENDA NA NANIHIII KAMA HIZI KWANI UKIFIKA NAZO KULE NI KIZAZAA KITUPU,HIVYO WENYE NAZO WALIANZA KUZITELEKEZA KWA BARABARA KAMA HIVI. UPO HAPOOO!!!!!!!!!!
Mangi mimi na uroha wa nyamazzzz niliumwaje tumboo!! nahisi nilikula hazijaiva vizuri,Usiulize kilichoendelea hapo shost nilitamani kurudia njiani. na ujue hapo ni siku ya tatu kwa barabara ni kusogea kiduchu na kulala.

Kilichonistaajabisha na kunishangaza ni jinsi maeneo yote barabara nzima ni kinyesi hapa,nyama choma pembeni,mwenye jiko lake kwa jirani hapo hapo,zile ngozi za mbusi na ngombe nazo zimetupwa hapo hapo ILA NZI NDIO HAMNA HATA MMOJA.

Maji sasa wasonjo wa kimasai wanafanya bizineee acha kabisa, hiyo ni chai iko jikoni na hiyo rangi ni ya maji wala sio majani,Na unakunywa tena kwa kugombania,Shost chooonde chonde ukienda ukumbuke kajiko baasi na maji ya kutosha,Ukijidai kujaza watu kwenye gari ujue itakula kwako,acha nafasi ya kuweka misosi.

Nyamazzzz inagombaniwa hapo



WAMASAI WANACHANGANYIKIWA NA CHAPAA WANALEWA HADI NANIHII WANAZISAHAU JUUU
Nimefurahi sana serikali yetu walivyositisha watu kwanda mpaka wafanye utaratibu flani,kwani kwa hali hii mlipuko wa magonjwa ulikuwa wa kufikia.

Mlima wa dawa huo kwa babu kikombe

Kaeni mtulie mkifanya fujo babu anastopisha kikombe.ila kila mtu atapata kikombe.


Baada ya kuchemsha dawa babu anatunza mazingira kwa kuyachoma makapi ya dawa

Babu house

Jamani ambao ndio mnajiandaa kwenda naomba muwapelekee zile kata za kuchotea dawa kwani wanaungua kweli wakati wa kuchota dawa.

Hemazz hizo!kulala elfu kumi tuu kwa kichwa.



Hatimae yulifika kwa babu tukapata kikombe baada ya kuhamua kuiacha gari na kutembea kwa tz 11 kwa miguu zaidi ya kilomita 20 hapo piki piki huwezi kupanda labda uwe umezidiwa na tofauti na hapo getini hupiti
.SHOST POLE KWA KUKOSA MATUKIO MENGINE MENGINE KWANI HUKO UKIONEKANA UKIPIGA PICHA NA UGOMVI KWELI SANA.ILA KIUKWELI NILIONA VITU VYA AJABU SANA WATU WANAUMWA SAAAANA NA ZAIDI KUNA NJEMBA MOJA ILIVYOKUNYWA TUU DAWA NYOKA ALICHOMOKA KWANYE SURUALI NA WAMASAI WAKAMUUA NA YEYE AKAFA HAPO HAPO.
dada kumbe na wewe hukuwa nyuma kupata mugariga